Kuchunguza Dhima ya Mtindo katika Tamthiliya za Kihistoria: Utafiti Linganishi wa Tamthiliya za Morani na Kinjeketile,

Fadhili, Fadhili Elifuraha (2014) Kuchunguza Dhima ya Mtindo katika Tamthiliya za Kihistoria: Utafiti Linganishi wa Tamthiliya za Morani na Kinjeketile,. Masters thesis, The Open University of Tanzania.

[thumbnail of DISSERTATION_FADHILI_E_FADHILI.pdf]
Preview
PDF
Download (627kB) | Preview

Abstract

Lengo la utafiti huu kama lilivyobainishwa katika sura ya kwanza ilikuwa ni kuchunguza dhima ya vipengele vya kimtindo katika tamthiliya za kihistoria kwa kulinganisha tamthiliya ya Morani na Kinjeketile ili kubaini vipengele vinavyowafananisha na kuwatofautisha wasanii wa vitabu hivyo katika kuliwasilisha suala la kihistoria. Utafiti huu ulitumia mbinu tatu za ukusanyaji data ambazo ni; maktaba, usaili na dodoso. Sampuli iliteuliwa kwa kutumia mbinu ya madhumuni maalumu na uteuzi rahisi. Aidha data za utafiti huu zilichambuliwa kwa kutumia mbinu ya uchambuzi maudhui na uchambuzi linganishi. Utafiti huu uliongozwa na Nadharia ya Elimumitindo katika Uchambuzi wa Matini za Kifasihi. Utafiti umegundua kuwa, tamthiliya hizi zinatofautiana katika mbinu za kisanii na ubunifu. Tamthiliya ya Morani imetumia mbinu na lugha ya kitamathali wakati tamthiliya ya Kinjeketile imetumia lugha ya kawaida, rahisi na ya wazi zaidi. Aidha utafiti huu umebaini kuwa, tamthiliya hizi zinatofutiana katika kuwasilisha suala la kihistoria kwa sababu wasanii wanawasilisha historia ya jamii ya Tanzania katika vipindi viwili tofauti. Morani anawasilisha historia katika kipindi cha baada ya uhuru na hivyo kujadili juu ya historia ya harakati za kupambana na ukoloni mamboleo wakati Kinjeketile inajadili kwa uhalisia juu ya harakati za jamii za kusini katika kupambana na ukoloni mkongwe, yaani, ukoloni katika utawala wa Mjerumani. Kwa upande mwingine, ilibainika kuwa tamthiliya hizi kwa vile zimeandikwa na wasanii wa jamii moja ambao wameshuhudia na kupata masimulizi ya historia ya jamii yao. Wasanii hawa wanafanana katika kuwasilisha maudhui ya kazi zao ambapo wote kwa pamoja wanajadili juu ya mambo mbalimbali yaliyopo katika jamii kama vile; rushwa, harakati za ukombozi, usaliti, unyonyaji na ukandamizaji.

Item Type: Thesis (Masters)
Subjects: 400 Language > 490 Other languages
Divisions: Faculty of Arts and Social Sciences > Department of Linguistics and Literary Studies
Depositing User: Mr Habibu Kazimzuri
Date Deposited: 14 Jan 2016 12:29
Last Modified: 14 Jan 2016 12:29
URI: http://repository.out.ac.tz/id/eprint/572

Actions (login required)

View Item View Item