Rashid, Mwajabu Majaliwa
(2025)
Kuchunguza Ujumbe Unaojengwa na Muktadha katika Nyimbo za Asili za Sherehe za Wahehe.
Masters thesis, The Open University of Tanzania.
Abstract
Utafiti huu ulilenga “Kuchunguza ujumbe unaojengwa na muktadha katika nyimbo za asili za sherehe za Wahehe,” kwa kuongozwa na malengo mahususi mawili: kubainisha miktadha ya uwasilishaji wa nyimbo za asili za sherehe za Wahehe na kuelezea ujumbe unaopatikana katika nyimbo za asili za Sherehe za Wahehe. Mbinu za ukusanyaji wa data ulihusisha mbinu za ushiriki kwenye shughuli za sherehe za za Wahehe, ushuhudiaji na hojaji. Utafiti huu unajengwa na nadharia ya Mwitiko wa Msomaji. Matokeo ya utafiti huu yanaonesha kwamba, nyimbo za asili za Sherehe za Wahehe hutumika katika Miktadha mbalimbali ya jamii hiyo kama vile: shughuli za ,matambiko,kilimo,misiba,jando na unyago,shghuli za ndoa ambapo mambo kadhaa hufanyika kama vile,kumuona binti, kuwatuma wazee kwenda nyumbani kwa wazazi wa binti kuzungumza nao, kuposa, kupangiwa mahari, kulipa mahari, kufanyiwa sherehe ya harusi, kwenda nyumbani na kuanza maisha ya ndoa. Aidha, nyimbo hizo zina ujumbe mzuri na muhimu kwa wanajamii wa asili ya Wahehe na Watanzania kwa ujumla, kwa kuwa Wahehe pia huoana na watu wengine wa maeneo ya nje na kabila lao. Utafiti umetoa mapendekezo zaidi kwa utafiti ujao katika eneo la fani katika nyimbo za harusi za jamii ya Wahehe hususani matumizi ya lugha kwani kuna utajiri mkubwa wa mbinu za matumizi ya lugha katika nyimbo hizo.
Actions (login required)
 |
View Item |