Uchunguzi wa Migongano ya Kimbari katika Muktadha wa Zanzibar ya Ubaadaukoloni: Uchanganuzi wa Riwaya ya Vuta N’kuvute na Mungu Hakopeshwi.

Ibrahim, Ulfat Abdulaziz (2023) Uchunguzi wa Migongano ya Kimbari katika Muktadha wa Zanzibar ya Ubaadaukoloni: Uchanganuzi wa Riwaya ya Vuta N’kuvute na Mungu Hakopeshwi. Masters thesis, The Open University of Tanzania.

[thumbnail of ULFAT ABDULAZIZ IBRAHIM.pdf] PDF - Submitted Version
Available under License Creative Commons Attribution.

Download (620kB)

Abstract

Tasinifu hii inahusu ‘Uchunguzi wa Migongano ya Kimbari katika Muktadha wa Zanzibar ya Ubaadaukoloni: Uchanganuzi wa Riwaya ya Vuta N’kuvute na Mungu Hakopeshwi’, Ili kutimiza kusudi hilo kulikuwa na malengo mahsusi matatu. Lengo la kwanza lilikuwa kubainisha makundi ya kimbari yanayoonekana katika jamii ya Zanzibar ya Baadaukoloni kupitia riwaya ya Vuta N’kuvute na Mungu Hakopeshwi, lengo la pili lilikuwa kuchanganua aina za migongano ya kimbari ya jamii ya Wazanzibari wa Baadaukoloni kupitia riwaya ya Vuta N’kuvute na Mungu Hakopeshwi na lengo la tatu lilikuwa kutathmini mikakati ya utangamano wa kimbari inayopendekezwa katika riwaya za Vuta N’kuvute na Mungu Hakopeshwi. Data za msingi zilikusanywa kwa mbinu ya usomaji makini na uchambuzi wa kinyaraka. Mjadala na uchambuzi wa data uliongozwa na nadharia ya Ubaadaukoloni. Matokeo ya utafiti yanaonesha kwamba katika riwaya teule kuna makundi ya kimbari ya kundi la Waafrika au Waswahili, kundi la Waarabu, kundi la Wahindi na kundi la Machotara. Kwa upande wa aina za migogoro ya Kimbari tumebaini aina mbili ambazo ni hisia-kinzani katika utambulisho na hisia-kinzani katika ndoa na mapenzi. Matokeo ya utafiti yanaendelea kuonesha kwamba mikakati ya kuondoa migongano hiyo ni kufanya mabadiliko ya tabia na utambulisho mpya wa Wanajamii kuwa na mapenzi yasiyokuwa na mipaka ya kimbari na uvunjaji wa mila za kinasaba. Utafiti huu unapendekeza utafiti zaidi katika eneo hili la umbari na fasihi ufanyike zaidi na pia kutoa elimu kwa umma juu ya watu wote kuishi kwa pamoja na kushirikiana katika mambo ya kijamii kutasaidia katika kupunguza na hata kuondoa migongano ya kimbari.

Item Type: Thesis (Masters)
Subjects: 400 Language > 490 Other languages
Divisions: Faculty of Arts and Social Sciences > Department of Linguistics and Literary Studies
Depositing User: Mr Habibu Kazimzuri
Date Deposited: 06 Sep 2024 10:25
Last Modified: 06 Sep 2024 10:25
URI: http://repository.out.ac.tz/id/eprint/4183

Actions (login required)

View Item View Item