Kuchunguza Tamathali za Semi katika Kuibua Dhamira katika Riwaya ya Mbali na Nyumbani

Mbarouk,, Issa Khamis (2017) Kuchunguza Tamathali za Semi katika Kuibua Dhamira katika Riwaya ya Mbali na Nyumbani. Masters thesis, The Open University of Tanzania.

[thumbnail of ISSA KHAMIS MBAROUK.pdf]
Preview
PDF - Submitted Version
Download (277kB) | Preview

Abstract

Utafiti huu unahusu uchunguzi wa tamathali za semi katika kuibua dhamira katika riwaya ya Shafi Adam Shafi. Mbali na Nyumbani. Lengo kuu la utafiti huu lilikuwa ni kuchunguza matumizi ya tamathali za semi katika riwaya ya Mbali na Nyumbani (2013) ya Shafi Adam Shafi, ili kuona jinsi gani tamathali zimetumika kisanii katika kuibua dhamira katika kazi hii. Sampuli ya utafiti huu iliteuliwa kwa kutumia mbinu ya uteuzi wa madhumuni maalum, wakati ambapo data zilikusanywa kwa kutumia mbinu ya mapitio ya maandishi. Data zilichambuliwa kwa kutumia mbinu ya uchambuzi maudhui. Uchunguzi, uchambuzi na mjadala wa matokeo ya utafiti huu yaliongozwa na nadharia ya Simiotiki.Matokeo ya utafiti huu yameonesha kuwa, Shafi Adam Shafi ametumia tamathali za semi kama mbinu ya kimtindo katika kuibua dhamira za kazi yake. Hii ni kusema kwamba Shafi Adam Shafi anaendelea kuitumia mbinu ya tamathali za usemi kama kibainishi chake cha mtindo katika kazi zake za riwaya. Riwaya ya Mbali na Nyumbani imeathiriwa zaidi na matumizi ya tashibiha ikifuatiwa na tashihisi na tamathali nyengine zimetumika katika kuongeza nguvu ya ufahamu wa riwaya hiyo.

Item Type: Thesis (Masters)
Subjects: 400 Language > 490 Other languages
Divisions: Faculty of Arts and Social Sciences > Department of Linguistics and Literary Studies
Depositing User: Mr Habibu Kazimzuri
Date Deposited: 29 Feb 2020 10:36
Last Modified: 29 Feb 2020 10:36
URI: http://repository.out.ac.tz/id/eprint/2441

Actions (login required)

View Item View Item