Matumizi ya Lugha na Dhamira katika Tamthilia Teule za Mwandishi Emmanuel Mbogo

Ali, Safinia Khamis (2017) Matumizi ya Lugha na Dhamira katika Tamthilia Teule za Mwandishi Emmanuel Mbogo. Masters thesis, The Open University of Tanzania.

[thumbnail of TASNIFU YA Safinia-30-01-2017.pdf]
Preview
PDF - Submitted Version
Download (548kB) | Preview

Abstract

Utafiti huu umeshughulikia matumizi ya lugha katika Tamthiliya Teule za mwandishi Emmanuel Mbogo pamoja na dhamira zilizojitokeza ndani ya utumizi huo wa lugha. Uchambuzi ulijikita katika malengo mahususi mawili ambayo ni kuchambua matumizi ya lugha katika tamthiiya teule za Emmanuel mbogo na kubainisha namna matumizi ya lugha yalivyojenga dhamira katika tamthiliya teule za Emmanuel Mbogo. Katika kukusanya data mtafiti alitumia mbinu ya Upitiaji wa nyaraka, kompyuta, Usomaji wa makini, uchambuzi wa data zilizochambuliwa kwa kutumia maswali yaliyowasilishwa mwanzoni pamoja na mbinu ya kimaelezo katika kuchambua data. Uchambuzi umeonesha kwamba matumizi ya lugha na dhamira zilizomo ndani ya tamthiliya teule za Emmanuel Mbogo zimejenga umahiri wa mtunzi pamoja na kwenda sambamba na muktadha husika kupitia utomeaji wa maneno teule, ubunifu wa hali ya juu, kuikuza na kuiendeleza lugha ya Kiswahili. Dhamira zilizomo katika uchanganuzi wa data ni kuchanganua matumizi ya lugha yalivyotumika kisanii kwa kuisana lugha ya kiswahii na kufikisha ujumbe uliokusudiwa kwa hadhira. Vile vile, utafiti umeonesha kwamba mbinu za kisanaa zilizotumiwa na mtunzi kwenye matumizi ya lugha ni nyingi ikiwemo, matumizi ya lugha kwa ujumla, utumizi wa tamathali za usemi kama vile semi, misemo, methali, lugha ya picha, takriri, tanakali sauti, lugha ya ishara, tashbiha, tash-hisi, mdokezo na mubalagha. Mwishoni mwa utafiti kumetolewa mapendekezo kwa ajili ya tafiti zijazo (za baadae) kwa kupitia utanzu wa fasihi Andishi kwa matumizi ya lugha ili kulipata pengo ambalo kalikupatiwa ufumbuzi na kulitafutia ufumbuzi kwa upande mwengine wa kazi za tamthiliya ambazo ni miongoni mwa kazi za fasihi kupitia lugha kupitia vipengele vyengine vya lugha.

Item Type: Thesis (Masters)
Subjects: 400 Language > 490 Other languages
Divisions: Faculty of Arts and Social Sciences > Department of Linguistics and Literary Studies
Depositing User: Mr Habibu Kazimzuri
Date Deposited: 05 Oct 2018 17:34
Last Modified: 05 Oct 2018 17:34
URI: http://repository.out.ac.tz/id/eprint/2126

Actions (login required)

View Item View Item