Uchambuzi wa Kiisimujamii Katika Majina ya Koo za Kisukuma: Mfano Wilaya ya Misungwi

Kalekwa, Leticia Bussungu (2018) Uchambuzi wa Kiisimujamii Katika Majina ya Koo za Kisukuma: Mfano Wilaya ya Misungwi. Masters thesis, The Open University of Tanzania.

[thumbnail of TASNIFU  YA SHAhadaDA YA UMAHIRI KATIKA KISWAHILI-MUSWADA WA MWISHO..pdf]
Preview
PDF - Submitted Version
Download (3MB) | Preview

Abstract

Utafiti huu ulilenga kuchambua kiisimujamii majina ya koo za kisukuma wilayani Misungwi katika mkoa wa Mwanza. Katika kutimiza azima hii, malengo mahususi yalikuwa kwanza, kufafanua jinsi majina ya kisukuma yanavyotofautisha jinsi ya wanajamii na kuchambua jinsi Nyanja za kiisimujamii zinavyosababisha majina ya koo hizo. Mikabala ya maelezo na takwimu imetumika. Mbinu za utafiti zilizotumika ni usaili na hojaji. Sampuli makusudi imetumika. Eneo la utafiti ni Wilaya ya Misungwi katika mkoa wa Mwanza. Data zimekusanywa kwa maswali dodoso, na usaili .Matokeo ya utafiti wa lengo mahususi la kwanza yamebainisha majina kutofautisha jinsi za wanajamii hawa lakini yanafanana kimaana, ijapokuwa yanatofautiana kifonolojia kutokana na kitamkwa (fonimu) kimoja au silabi moja inayounda maneno ya majina hayo. Mfano ―Kabula,‖ ni mwanamke wakati ―Mabula‖ ni mwamme, lakini yote mawili yanamaanisha ―Mvua‖. Kwahiyo, silabi $ka$ na $ma$ ndiyo hutofautisha jinsi hizi mbili.Aidha utafiti umedhihirisha kuwa, nyanja za kiisimujamii zinazotofautisha majina ya koo za kisukuma kisemantiki na kiisimujamii kama hapo juu, ilihali Kiisimu jamii yanazingatia matukio, ukoo mahali alipozaliwa, na baada ya kuzaliwa mtu. Mfano, ―Bulugu‖ au ―Malugu‖ hutokana na vita(vurugu). Kiukoo, jina ―Ng‘hwashi‖ inamaanisha ukoo wa wavuvi ili hali ―Ngwandu‖ inamaanisha aliyezaliwa chini ya Mbuyu.Utafiti umehitimisha kuwa , majina ya koo za kisukuma yanafanana kimaana, lakini yanatofautiana kifonolojia kuhusu jinsi. Aidha, majina ya koo za kisukuma yamegawanyika katika vigezo vya kisemantiki na kiisimujamii.

Item Type: Thesis (Masters)
Subjects: 400 Language > 490 Other languages
Divisions: Faculty of Arts and Social Sciences > Department of Linguistics and Literary Studies
Depositing User: Mr Habibu Kazimzuri
Date Deposited: 05 Oct 2018 17:32
Last Modified: 05 Oct 2018 17:32
URI: http://repository.out.ac.tz/id/eprint/2125

Actions (login required)

View Item View Item