Athari ya Kimakunduchi Katika Kiswahili Sanifu

Bundalla, Rukia Ramadhan (2017) Athari ya Kimakunduchi Katika Kiswahili Sanifu. Masters thesis, The Open University of Tanzania.

[thumbnail of Rukia's TASNIFU-01-11-2017 final.pdf]
Preview
PDF - Submitted Version
Download (906kB) | Preview

Abstract

Utafiti huu ulichunguza athari za lahaja ya Kimakunduchi katika Kiswahili sanifu. Utafiti huu ulitumia muundo wa kimaelezo na majadweli. Sampuli iliyotumika ni sampuli nasibu rahisi. Eneo la utafiti ni Mkoa wa Kusini Unguja. Mbinu zilizotumika kukusanya data ni dodoso, usaili pamoja na mahojiano. Utafiti huu umebaini kuwa baadhi ya wazungumzaji wa Kimakunduchi, wanatumia makundi ya kijamii yanayotumia vipengele vya Kimakunduchi katika Kiswahili sanifu ni pamoja na wazee, vijana, walimu na wanafunzi. Sababu za kutumia vipengele hivyo zinatokana na kuathiriwa na lugha ya kwanza. Utafiti ulihitimisha kuwa lahaja ya Kimakunduchi na Kiswahili sanifu ni lahaja zinazotumika katika mawasiliano kwa wakaazi wa visiwa vya Unguja. Imebainika kuwa kuna misamiati inayofanana na misamiati inayotafautiana ambayo huleta vikwazo katika mawasiliano katika makundi hayo mawili. Mwisho utafiti huu unapendekeza watafiti wengine kufanya utafiti zaidi katika maeneo ya kimuundo, kimsamiati pamoja na athari za matamshi ya Kimakunduchi katika Kiswahili sanifu kuingizwa katika shughuli rasmi.

Item Type: Thesis (Masters)
Subjects: 400 Language > 490 Other languages
Divisions: Faculty of Arts and Social Sciences > Department of Linguistics and Literary Studies
Depositing User: Mr Habibu Kazimzuri
Date Deposited: 05 Oct 2018 16:19
Last Modified: 05 Oct 2018 16:19
URI: http://repository.out.ac.tz/id/eprint/2104

Actions (login required)

View Item View Item