Matumizi ya Lugha Tandawazi katika Mitandao ya Kijamii, Changamoto katika Lugha ya Kiswahili

Faki, Miza Hassan (2018) Matumizi ya Lugha Tandawazi katika Mitandao ya Kijamii, Changamoto katika Lugha ya Kiswahili. Masters thesis, The Open University of Tanzania.

[thumbnail of MIZA HASSAN FAKI-TASNIFU-10-02-2018.pdf]
Preview
PDF - Submitted Version
Download (759kB) | Preview

Abstract

Utafiti huu ulichunguza Matumizi ya Lughatandawazi katika Mitandao ya Kijamii, Changamoto zake katika Lugha ya Kiswahili. Utafiti umefanyika Kisiwani Pemba. Jumla ya watafitiwa 80 waliolengwa kufanyiwa utafiti watafitiwa 75 ndio walioshiriki katika utafiti huu. Utafiti huu ulihusisha makundi ya vijana na wazee wanaoishi katika miji ya Wilaya hizi. Malengo ya utafiti yalikuwa ni kubainisha aina za lughatandawazi zinazotumika katika mitandao ya kijamii. Kubainisha sababu zinazopelekea utumiaji wa lugha tandawazi katika mitandao ya kijamii. Kufafanua athari za matumizi ya lugha tandawazi katika lugha ya Kiswahili. Data zimekusanywa kwa kutumia mbinu ya usaili hojaji na ushuhudiaji na zimechambuliwa kwa mkabala wa kiidadi na usio wa kiidadi na kuongozwa na Nadharia Kidhi ya Mawasiliano. Utafiti huu umeundwa kwa sura tano, ambazo ni utangulizi, mapitio ya kazi tangulizi na kiunzi cha nadharia, njia na mbinu za utafiti, sura ya kuchanganua data za utafiti na muhtasari, hitimisho na mapendekezo. Matokeo yameonesha kuwa ujumbe unaoandikwa kwenye mitandao ya kijamii unatumia mitindo yenye lugha tandawazi. Sababu walizoeleza watafitiwa za kutumia mtindo huu ni pamoja na kuokoa muda, wepesi na urahisi wa kuandika, kwenda na wakati na kuonesha ubunifu wa maneno. Aidha watafitiwa wametoa maoni yao kwa kusema mtindo huu una athari hasi katika lugha ya Kiswahili. Athari zenyewe ni za kiisimu na zisizo na isimu. Kadhalika watafitiwa wametoa mapendekezo kwa kusema kuwa itolewe elimu katika jamii juu ya athari za utumiaji wa mitindo kama hii. Aidha, kuwepo na taasisi maalum zitakazofuatilia na kupiga marufuku utumiaji wa mitindo kama hii.

Item Type: Thesis (Masters)
Subjects: 400 Language > 490 Other languages
Divisions: Faculty of Arts and Social Sciences > Department of Linguistics and Literary Studies
Depositing User: Mr Habibu Kazimzuri
Date Deposited: 05 Oct 2018 14:18
Last Modified: 05 Oct 2018 14:18
URI: http://repository.out.ac.tz/id/eprint/2088

Actions (login required)

View Item View Item