Mtindo katika Riwaya ya Marimba ya Majaliwa ya Edwin Semzaba

Silavwe, Martha Isaack (2016) Mtindo katika Riwaya ya Marimba ya Majaliwa ya Edwin Semzaba. Masters thesis, The Open University of Tanzania.

[thumbnail of TASINIFU_YA_MARTHA_23-12-2016-2.pdf]
Preview
PDF - Submitted Version
Download (382kB) | Preview

Abstract

Lengo kuu la utafiti huu lilikuwa ni kuchambua matumizi ya mtindo katika riwaya ya Marimba ya Majaliwa. Malengo mahususi yalikuwa mawili ambayo ni kuchambua matumizi ya mtindo yanayohusiana na lugha katika riwaya ya Marimba ya Majaliwa na kubainisha matumizi ya mtindo yanayohusiana na vipengele vinginevyo vya kimtindo katika riwaya ya Marimba ya Majaliwa. Data za utafiti zimekusanywa kwa kutumia mbinu za usomaji makini na upitiaji wa nyaraka. Data hizo zilizokusanywa zilichambuliwa kwa kutumia mkabala wa kimaelezo na nadharia ya Simiotiki. Kwa upande wa lengo mahususi la kwanza, matokeo ya utafiti yanabainisha kuwa matumizi ya kimtindo ya lugha ni pamoja na tamathali za usemi za tashibiha, chuku na takriri. Pia kuna matumizi ya methali na Kiswahili cha kimaeneo. Kwa upande wa lengo mahususi la pili, matokeo ya utafiti ni kuwa vipengele vingine vya kimtindo vilivyotumika katika riwaya teule ni matumizi ya nyimbo, hadithi ndani ya hadithi, mwingiliano matini, tanzu ndani ya tanzu ndani ya tanzu na uhalisia mazingaombwe.

Item Type: Thesis (Masters)
Subjects: 400 Language > 490 Other languages
Divisions: Faculty of Arts and Social Sciences > Department of Linguistics and Literary Studies
Depositing User: Mr Habibu Kazimzuri
Date Deposited: 14 Feb 2017 12:34
Last Modified: 23 May 2017 12:09
URI: http://repository.out.ac.tz/id/eprint/1612

Actions (login required)

View Item View Item