Kuchambuwa Maudhui ya Hadithi za Watoto Katika Jamii ya Wapemba

Mzee, Mwanaika Madi (2015) Kuchambuwa Maudhui ya Hadithi za Watoto Katika Jamii ya Wapemba. Masters thesis, The Open University Of Tanzania.

[thumbnail of Dissertation_for_MA-Kiswahili_Mwanaika_Madi_Mzee_-_Final.pdf]
Preview
PDF
Download (602kB) | Preview

Abstract

Kazi hii ilihusika na hadithi za Paukwa…. Pakawa. Imechunguza maudhui yanazopatikana katika hadithi za watoto katika jimbo la Mkanyageni Mkoa wa kusini Pemba. Ili kufikia lengokuu lililokusudiwa mbinu mbalimbali za utafiti zilihusika. Mbinu hizo ni za mahojiano pamoja na uchunguzi wa kimaktaba. Nadharia tatu za utafiti zilitumika. Nadhariza hizo ni mwitiko wa msomaji, nadharia ya simiotiki na nadharia ya sosholojia (kijamii).Kwa upande wa matokeo ya utafiti, mtafiti amegunduwa dhamira kadha wa kadha zilizoibuka kutokana na utafiti na uchambuzi alioufanya. Dhamira hizo ni ugumu wa upatikanaji wa elimu, umoja na mshikamano miongoni mwa wanajamii. mapenzi na ndoa, kuonya,nafasi ya mwanamke, ukarimu, uzembe na uvunjaji wa kanuni pamoja na utawala bora. Kifani, mtafiti amegundua kwamba, baadhi ya vipengele vya fani vilivyosaidia kuibua dhamira katika hadithi za watoto za Kipemba ni kipengele kinachohusu wahusika, matumizi ya lugha, muundo, mtindo na mandhari.Ujumbe uliojitokeza katika hadithi za watoto ni pamoja na wazee kuwaasa watoto juu ya kufuata ushauri wa wazazi wao kwa kila wanalotaka kulifanya, kujitenga na mambo mbalimbali ambayo yanaweza kukuletea vikwazo au matatizo, wanataalimu wawe wavumilivu, wasiwe na ufedhuli na lugha chafu kwa wanafunzi wao. Ujumbe mwengine uliopatikana ni kuwa na juhudi ya kazi na kuwacha kujigamba pasipo sababu, kutokuwa na imani na kila mtu,kuepuka ubinafsi na ujanja katika kazi, kutii kanuni na utii wa wake na waume zao na kuepuka ushawishi wa mashoga na watu wengine.

Item Type: Thesis (Masters)
Subjects: 400 Language > 490 Other languages
Divisions: Faculty of Arts and Social Sciences > Department of Linguistics and Literary Studies
Depositing User: Mr Habibu Kazimzuri
Date Deposited: 13 Jul 2016 10:27
Last Modified: 13 Jul 2016 10:27
URI: http://repository.out.ac.tz/id/eprint/1339

Actions (login required)

View Item View Item