Muhidin, Faida Fakih
(2025)
Taswira za ushujaa na uzalendo zinavyoibuwa hali halisi ya kisiasa katika maisha: Tamthilia teule za Emmanuel Mbogo.
Masters thesis, The Open University of Tanzania.
Abstract
Utafiti huu umelenga kuchunguza taswira za ushujaa na uzalendo zinavyoibua hali halisi ya kisiasa katika maisha kupitia tamthilia za Emmanuel Mbogo za Nyerere na Safari ya Kanaani na Mondlane na Samora. Utafiti umeongozwa na malengo mahasusi matatu ambayo ni; kubainisha taswira zilizotumika katika tamthilia teule za Mbogo; kuchambua aina za taswira zinazowasilisha dhamira za uzalendo na ushujaa katika tamthilia teule za Mbogo pamoja na kuchambua jinsi taswira za ushujaa na uzalendo zinavyosawiri hali halisi ya kisiasa katika tamthilia za Mbogo. Utafiti huu umeongozwa na nadharia ya Simiotiki. Matokeo ya utafiti yamebaini kuwa zipo taswira mbalimbali katika tamthilia hizi zinazohusiana na uzalendo na ushujaa. Katika lengo la kwanza, utafiti umeonesha taswira kama vile, taswira za utungu na maumivu ya Wanaafrika ambazo zilionesha matatizo yaliyowakumba Wanamsumbiji katika kupigania uhuru kutoka katika tamthilia ya Mondlane na Samora na taswira za misimamo ya mwalimu Nyerere katika kusimamia siasa za ujamaa katika tamthilia ya Nyerere na Safari ya kanaani. Lengo la pili limebainisha aina mbalimbali za taswira na namna zilivyoweza kutoa sura ya maisha na mapitio ya nchi za Kiafrika kabla na mara tu baada ya uhuru wanchi hizo kama ilivyooneshwa kwa nchi za Msumbiji (kabla ya uhuru) na Tanzania (baada ya uhuru). Lengo la tatu limechambua na kuonesha jinsi taswira zilizochambuliwa katika malengo mawili yaliyotangulia zilivyosawiri hali halisi ya kisiasa.
Maneno Makuu: Taswira, Simiotiki, Uzalendo
Actions (login required)
 |
View Item |