Michakato na Mbinu Zilizotumika Katika Uundaji wa Majina ya Mitaa Katika Wilaya ya Mjini Unguja

Rashid, Moza Omar (2017) Michakato na Mbinu Zilizotumika Katika Uundaji wa Majina ya Mitaa Katika Wilaya ya Mjini Unguja. Masters thesis, The Open University of Tanzania.

[thumbnail of TASINIFU YA MOZA OMAR -31-10-2017 .pdf]
Preview
PDF - Submitted Version
Download (1MB) | Preview

Abstract

Tasnifu hii inawasilisha uchunguzi uliofanywa kuhusu michakato na mbinu zilizotumika katika uundaji wa maneno ya mitaa mbalimbali katika wilaya ya Mjini Unguja. Malengo mahususi yalikuwa ni pamoja na kubainisha vigezo, kuelezea michakato iliyotumika kupata majina hayo, na kubainisha umuhimu wa majina ya mitaa katika kukuza lugha ya Kiswahili. Utafiti ulitumia muundo wa maelezo na takwimu Utafiti ulifanyika katika wilaya ya Mjini Unguja. Walengwa wa utafiti walikuwa ni wakaazi wa wilaya ya Mjini Unguja. Usampulishaji ulifanywa kwa kutumia njia ya usampulishaji tabakishi. Jumla ya watafitiwa 90 walihusishwa katika utafiti huu. Ukusanyaji wa data ulifanywa kwa kutumia njia za mahojiano (usaili), uchunguzi makini, dodoso na mapitio ya nyaraka. Matokeo ya utafiti yanaonesha kuwa; vigezo vilivyotumika katika kutoa majina ya mitaa katika wilaya ya Mjini Unguja ni vya kimaumbile, kijamii na kiuchumi.. Utafiti umeonesha kuwa njia ambayo imetumika zaidi katika kuita majina ya mitaa katika wilaya ya Mjini Unguja ni njia ya uambatishaji wa maneno. Majina hayo ya mitaa yamechangia sana katika kuleta misamiati mipya hasa ya maneno ambatano. Utafiti umeonesha pia kuwa maneno ambayo yametumika kuita majina ya mitaa katika wilaya ya Mjini Unguja yametokana na miundo mbalimbali ya maneno na muundo uliotumika zaidi ni mwambatano wa nomino na nomino. Utafiti umedhihirisha pia kuwa majina ya mitaa yameweza kudumisha maneno ya Kiswahili yenye hadhi kubwa kwenye lugha ya Kiswahili na kuhifadhi historia na urithi wa lugha yetu

Item Type: Thesis (Masters)
Subjects: 400 Language > 490 Other languages
Divisions: Faculty of Arts and Social Sciences > Department of Linguistics and Literary Studies
Depositing User: Mr Habibu Kazimzuri
Date Deposited: 05 Oct 2018 17:17
Last Modified: 05 Oct 2018 17:17
URI: http://repository.out.ac.tz/id/eprint/2120

Actions (login required)

View Item View Item