Sheha, Mwanakombo Mwadini
(2025)
Uchunguzi wa Mtindo katika kasida za Dufu za Kiislamu.
Masters thesis, The Open University of Tanzania.
Abstract
Utafiti huu ulichunguza “Uchunguzi wa Mtindo ya Kasida za Dufu za Kiislamu”. Mtafiti aliongozwa na malengo mahsusi matatu nayo ni Kufafanua mitindo ya kasida za dufu za Kiiislamu katika madrasa teule, Kuchambua mitindo ya kasida za dufu za Kiislamu iliyojitokeza katika kasida teule na Kubainisha namna mitindo ya kasida ya Kiislamu ilivyoibua dhamira. Malengo haya yaliukamilisha utafiti hatua kwa hatua katika kugundua mitindo ya kasida za dufu za Kiislamu. Mtafiti alikusanya data kupitia nyanjani katika madrasa tafauti zilizopo wilaya ya Mjini katika Mkoa wa Mjini Magharibi. Mtafiti aliwagawa watafitiwa katika makundi ya watunzi, walimu na wanafunzi. Kwa upande wa ukusanyaji na uchambuzi wa data za utafiti mtafiti aliongozwa na nadharia ya Mwitiko wa Msomaji, Upokezi na Umitindo. Aidha, matokeo ya utafiti huu yamethibitisha kuwapo kwa mitindo ya kasida za dufu za Kiislamu katika madrasa teule ambayo ni mtindo wa Ajmi, Bayati, Sika/Hijazi, Razdi/rasti, Muundo wa neno moja, mtindo wa mshangao, mtindo wa takriri, mtindo wa kutumia nafsi kwanza, ya pili, umoja ya pili wingi, na nafsi ya tatu umoja. Pia utafiti uligundua kuwapo kwa mtindo wa matumizi ya lugha ya tash-biha, sitiari, tash-hisi, taswira, tanakalisauti, mdokezo, nidaa, tafsida, hutuba na swali. Dhamira zilizoibuliwa na mtindo katika kasida ni zile za kijamii, kimapenzi, utukufu, upekee, majonzi, ukiwa, wasifu, mwitiko, ushajihisho, unyenyekevu, nasaha, kukumbushana, hamasa, ushawishi, kujikubalisha, kujimithilisha, uthibitisho na usaili. Mwisho, utafiti umependekeza watunzi wa kasida za dufu waendelee kutunga kasida nyingine zenye maudhui mbalimbali ili watafiti waweze kuibua mitindo, mbalimbali itakayokuza na kuendeleza fasihi ya Kiswahili.
Actions (login required)
 |
View Item |