Falsafa za Nyimbo za Harusi za Kimakunduchi katika kudumisha Ndoa.

Haji, Ilyas Nassib (2025) Falsafa za Nyimbo za Harusi za Kimakunduchi katika kudumisha Ndoa. Masters thesis, The Open University of Tanzania.

[thumbnail of TASNIFU YA ILYAS KWA AJILI YA BLACK BOOK.docx] PDF - Submitted Version
Available under License Creative Commons Attribution.

Download (309kB)
Official URL: http://www.out.ac.tz

Abstract

Wamakunduchi wanatumia Nyimbo za harusi kama njia ya kuwafunda wanandoa wao. Nyimbo hizo zinakuwa na msaada mkubwa katika mila na desturi walizojiwekea katika kudumisha ndoa. Mtafiti amefanya utafiti kwa lengo la kuchunguza falsafa za nyimbo za harusi za Kimakunduchi katika kudumisha ndoa, katika Shehia tatu ambazo ni Kiongoni, Kajengwa na Ng’anani. Watoa taarifa walikuwa ni wakaazi wa Makunduchi. Utafiti ulikusanya data kwa mbinu ya Usaili wa nusu kimuundo (Semi Structured Interview) na kupitia Machapisho. Nadharia ya uhalisia imetumika katika utafiti huu kutokana na kuonyesha uhalisia wa maisha jinsi yalivyo kulingana na falsafa zinazoibuliwa kupitia Nyimbo hizo zikiwa na lengo kuu la kudumisha ndoa. Data zilizokusanywa ni zile zinazozungumzia Maadili, nidhamu, suala la unyumba, kujenga udugu katika familia na kukemea maovu katika ndoa. Matokeo ya utafiti huu yanaonyesha wazi kuwa nyimbo za harusi zina falsafa kubwa ya kudumisha ndoa kwa wanajamii wa Makunduchi na Watanzania kwa ujumla.

Item Type: Thesis (Masters)
Subjects: 400 Language > 490 Other languages
Divisions: Faculty of Arts and Social Sciences > Department of Linguistics and Literary Studies
Depositing User: Mr Habibu Kazimzuri
Date Deposited: 30 Jan 2026 14:53
Last Modified: 30 Jan 2026 14:53
URI: http://repository.out.ac.tz/id/eprint/5005

Actions (login required)

View Item View Item