Athari za Mofu Ambishi na Nyambulishi katika Uundaji wa Vitenzi vya Kisambaa

Ally, Nasra Habibu (2020) Athari za Mofu Ambishi na Nyambulishi katika Uundaji wa Vitenzi vya Kisambaa. ["eprint_fieldopt_thesis_type_phd" not defined] thesis, The Open University of Tanzania.

[thumbnail of NASRA HABIBU ALLY THESIS tyr.pdf] PDF
Download (657kB)

Abstract

Utafiti huu umechunguza na kuchanganua kuathiriana kwa mofu ambishi na nyambulishi katika uundaji wa vitenzi vya Kisambaa. Katika uchunguzi na uchanganuzi huo, utafiti huu pia umedhihirisha mashartizuizi yanayotawala uambikaji wa mofu katika kitenzi cha Kisambaa. Uchambuzi na uwasilishaji wa data, katika utafiti huu umefanywa kwa kuongozwa na Nadharia ya Umbo Upeo iliyoasisiwa na Prince na Smolesky. Data za utafiti huu zilikusanywa kutoka tarafa ya Mlalo Wilaya ya Lushoto, maeneo ambako Wasambaa wanapatikana. Data hizo zilikusanywa kwa kutumia mbinu ya usaili na usomaji wa maandiko. Utafiti huu umebaini kuwa mofu ambishi na mofu nyambulishi zinapoambikwa katika mzizi wa kitenzi cha lugha ya Kisambaa zinaathiriana. Kuathiriana huko kumebainishwa kwa kuzingatia mashartizuizi yanayotawala mfuatano na mpangilio wa mofu katika kitenzi cha Kisambaa. Mofu ambishi na nyambulishi ambazo huathiriana ni pamoja na mofu ya mofimu ya njeo, ukanushi, masharti, kutendea, utendeshi, ufanyikaji sana, kutendeka na mofu ya mofimu ya urejeshi. Mofu hizo huathiriana katika kudondoshwa kwa mofu, kubadili nafasi ya utokeaji wa mofu na kubadilika kwa umbo la mofu inayoathiriwa pale zinapokaa pamoja kuunda kitenzi chenye maumbo mbalimbali yanayokubalika katika Kisambaa. Matokeo ya kuathiriana huko ni kupatikana kwa maumbo mbalimbali ya vitenzi yenye fahiwa tofauti tofauti. Maumbo hayo ya vitenzi yenye mabadiliko ni kama vitenzi vyenye ukanushi, masharti, vitenzi katika hali ya kutendwa, kutendea, urejeshi na utendeshi. Aidha, utafiti huu unapendekeza kuwa tafiti nyingine katika lugha ya Kisambaa kuhusu maumbo ya vitenzi na namna mofu zinavyoweza kuathiriana kisemantiki na kisintaksia zinahitajika. Vilevile kuna haja ya kuzitafiti zaidi lahaja katika lugha ya Kisambaa. Pamoja na hayo suala la toni katika lugha ya Kisambaa ni muhimu litafitiwe kwa kina.

Item Type: Thesis (["eprint_fieldopt_thesis_type_phd" not defined])
Subjects: 400 Language > 490 Other languages
Divisions: Faculty of Arts and Social Sciences > Department of Linguistics and Literary Studies
Depositing User: Mr. Administrator OUT
Date Deposited: 12 Apr 2021 07:21
Last Modified: 12 Apr 2021 07:21
URI: http://repository.out.ac.tz/id/eprint/2678

Actions (login required)

View Item View Item