Ulinganishi wa Tabia za Wahusika Wakuu na Dhamira Katika Riwaya za Kusadikika na Utengano

Moh'd, Miza Omar (2017) Ulinganishi wa Tabia za Wahusika Wakuu na Dhamira Katika Riwaya za Kusadikika na Utengano. Masters thesis, The Open University of Tanzania.

[thumbnail of TASNIFU-MIZA OMAR.pdf]
Preview
PDF - Submitted Version
Download (547kB) | Preview

Abstract

Lengo la utafiti huu lilikuwa ni kulinganisha tabia za wahusika wakuu nadhamira katika riwaya ya Kiswahili kwa kutumia mifano kutoka riwaya ya Kusadikika na Utengano. Pia, malengo mahususi yalikuwa matatu; ambayo ni kueleza muhutasari wa riwaya za Kusadikika na Utengano, kubainisha tabia za wahusika wakuu wa riwaya za Kusadikika na Utengano na kulinganisha tabia za wahusika wakuu wa riwaya za Kusadikika na Utengano. Data ya utafiti huu imekusanywa kutoka maktabani na uwandani. Kwa upande wa data za maktabani zimekusanywa kwa kutumia mbinu ya usomaji maandiko na data za uwandani zimekusanywa kwa kutumia mbinu tatu za ukusanyaji data. Mbinu hizo ni majadiliano ya vikundi, usaili na hojaji. Nadharia ya Uhalisia na Nadharia ya Uasilia zimetumika katika ukusanyaji na uchambuzi wa data za utafiti huu. Matokeo ya utafiti huu yameonesha kuwa wahusika wakuu katika riwaya zote mbili ya Kusadikika na Utengano, wamesawiriwa katika tabia za aina mbili; yaani tabia nzuri na tabia mbaya kwa wahusika hao. Pia, waandishi wa riwaya mbili hizi wameathiriwa na mapokeo simulizi ya visakale vya watu wa pwani. Riwaya zote mbili ya Kusadikika na Utengano zinafanana, sambamba na kutofautiana. Zaidi ya hayo, utafiti huu umebaini kuwa waandishi kwa kiasi kikubwa wanawatumia wahusika wakuu kuwasawiri matendo ya watu katika jamii inayohusika. Wahusika wakuu hao wengine hupambwa kwa tabia nzuri na wengine huvikwa tabia mbaya ili kuakisi tabia za binadamu katika jamii. Mwisho kabisa utafiti huu umetoa hitimisho la jumla na mapendekezo kwa watafiti wengine watakaopenda kuchunguza tabia za wahusika wakuu katika kazi za fasihi.

Item Type: Thesis (Masters)
Subjects: 400 Language > 490 Other languages
Divisions: Faculty of Arts and Social Sciences > Department of Linguistics and Literary Studies
Depositing User: Mr Habibu Kazimzuri
Date Deposited: 05 Oct 2018 17:37
Last Modified: 05 Oct 2018 17:37
URI: http://repository.out.ac.tz/id/eprint/2127

Actions (login required)

View Item View Item