Kuchunguza Matumizi ya Mbinu za Kisanaa na Dhamira katika Tamthiliya ya Morani

Abourweeshah, Abdulhadi Mohamed Abdulhadi (2017) Kuchunguza Matumizi ya Mbinu za Kisanaa na Dhamira katika Tamthiliya ya Morani. Masters thesis, The Open University of Tanzania.

[thumbnail of Tasinifu ya Abdulhadi -09-10-2017.pdf]
Preview
PDF - Submitted Version
Download (435kB) | Preview

Abstract

Lengo kuu la utafiti huu lilikuwa ni kuchunguza matumizi ya mbinu za kisanaa katika tamthiliya ya Morani. Ili kutimiza lengo hili kuu tulikuwa na malengo mahususi matatu; kuchambua matumizi ya mbinu za kisanaa za tamathali za usemi katika tamthiliya ya Morani, kuelezea matumizi ya mbinu za kisanaa zisizo tamathali za usemi katika tamthiliya ya Morani na kubainisha dhamira zitokanazo na matumizi ya mbinu za kisanaa katika tamthiliya ya Morani. Data za utafiti zilikusanywa kwa kutumia mbinu za usomaji makini na upitiaji wa nyaraka. Uchambuzi wa data umefanywa kwa kutumia mbinu ya mkabala wa kimaelezo na nadharia za Simiotiki na Korasi. Malengo mahususi matatu ya utafiti huu yalitimizwa vizuri ambapo kwa upande wa mbinu za kisanaa za tamathali za usemi tumechambua tamathali nne ambazo ni tashibiha, mbalagha, takriri na usambamba. Mbinu za kisanaa zisizo tamathali za usemi ni matumizi ya wahusika, wimbo, wahusika wa kikorasi na motifu. Kwa upande wa dhamira zitokanazo na matumizi ya mbinu za kisanaa tumebaini dhamira za uongozi na uhujumu uchumi, ugumu wa maisha, matabaka na haki na usawa.

Item Type: Thesis (Masters)
Subjects: 400 Language > 490 Other languages
Divisions: Faculty of Arts and Social Sciences > Department of Linguistics and Literary Studies
Depositing User: Mr Habibu Kazimzuri
Date Deposited: 05 Oct 2018 17:13
Last Modified: 05 Oct 2018 17:13
URI: http://repository.out.ac.tz/id/eprint/2119

Actions (login required)

View Item View Item