Kutathmini Ufasihi Simulizi katika Uandishi wa Ebrahim Hussein: Mfano wa Mashetani, Jogoo Kijijini na Ngao ya Jadi

Abdallah, Salum (2018) Kutathmini Ufasihi Simulizi katika Uandishi wa Ebrahim Hussein: Mfano wa Mashetani, Jogoo Kijijini na Ngao ya Jadi. Masters thesis, The Open University of Tanzania.

[thumbnail of SALUM ABDALLAH-TASNIFU-13-02-2018.pdf]
Preview
PDF - Submitted Version
Download (558kB) | Preview

Abstract

Utafiti huu umetathmini ufasihi simulizi katika uandishi wa Ebrahim Hussein: Mfano wa Jogoo Kijijni, Ngao ya Jadi na Mashetani. Utafiti huu uliongozwa na malengo mahsusi matatu ambayo ni kubainisha vipengele vya Fasihi simulizi katika tamthiliya za Jogoo Kijijni, Ngao ya Jadi na Mashetani, mwisho ni kubainisha namna vipengele vya fasihi simulizi vinavyoibua dhamira na kuendeleza dhamira mbalimbali katika tamthiliya teule. Katika kutekeleza malengo hayo tuliteua sampuli ya utafiti kwa mbinu ya kusudio. Sampuli hiyo ndiyo iliyotumiwa kukusanyia data ya msingi. Data hizi zilikusanywa kwa kutumia mbinu ya usomaji wa matini na kuchambuliwa kwa mkabala wa kimaelezo. Uhakiki wa data katika Utafiti huu uliongozwa na nadhariya mbili ambazo ni nadhariya ya Vikale ambayo imetumika kubainisha ufasihi simulizi katika tamthiliya teule. Na nadhariya ya Fasihi Linganishi imetumika kulinganisha na kulinganua ufasihi simulizi uliojitokeza katika tamthiliya teule. Matokeo ya uatafiti huu yameonyesha kwamba, mosi kuna ufanano mkubwa wa utumizi wa vipengele vya ufasihi simulizi katika tamthiliya teule mbapo katika tamthiliya zote tatu Hussein ametumia ngano, majigambo, ishara, mtindo wa kuchanganya tanzu, tashihisi, ushairi mtambaji, wahusika wa fasihi simulizi na mtambaji katika ujenzi wa tamthiliya ya Mashetani, Jogoo Kijijini na Ngao ya Jadi. Pili, Utafiti huu umebaini kuwa utofauti wa utumizi wa vipengele vya ufasihi simulizi umejitokeza kupitia kipengele cha nyimbo na mianzo na miisho ya kifomula. Vipengele hivi ndivyo livyozitofautisha tamthiliya teule.

Item Type: Thesis (Masters)
Subjects: 400 Language > 490 Other languages
Divisions: Faculty of Arts and Social Sciences > Department of Linguistics and Literary Studies
Depositing User: Mr Habibu Kazimzuri
Date Deposited: 29 Sep 2018 13:10
Last Modified: 29 Sep 2018 13:10
URI: http://repository.out.ac.tz/id/eprint/1994

Actions (login required)

View Item View Item