Kuchunguza Dhamira za Nyimbo za Siti Bint Saad

khamis, Wahida Ameir (2016) Kuchunguza Dhamira za Nyimbo za Siti Bint Saad. Masters thesis, The Open University of Tanzania.

[thumbnail of WAHIDA_1_New1.docx] PDF
Download (104kB)

Abstract

Utafiti huu umeshughulikia dhamira za nyimbo za Siti binti Saad. Ili kukamilisha lengo kuu, madhumuni mahususi mawili yalitimizwa. Madhumuni hayo yalihusu kuchunguza na kutathmini dhamira za nyimbo za Siti binti Saad na kubainisha mbinu za kisanii zilizotumiwa na msanii huyo katika kuibua dhamira. Mtafiti ametumia mbinu za uchambuzi wa kifasihi, usaili katika kukusanya data za utafiti. Mikabala ya kimaelezo na ule wakifasihi ndiyo iliyotumika katika kuchambua data za utafiti wetu.Kwa jumla, utafiti umeweza kukusanya data ambazo zimeweza kujibu maswali yaliyoulizwa kutokana na madhumuni mahsusi yautafiti huu ambapo imedhihirika kwamba, nyimbo za Siti binti Saad zimeshehenidhamira za matabaka utamaduni na mapenzi.Pia imebainika kwamba mbinu za kisanaa zimetumika kujenga dhamira, miongoni mwa dhamira zilizoibuliwa na matabaka utamaduni na mapenzi. Mbinu za kisaniizilizotumika ni kama mbinu ya simulizi, takriri, tashbiha, tash-hisi, ishara, misemo na muingiliano wa tanzu. Mwishoni mwa utafiti, kumetolewa mapendekezo kwa ajili ya tafiti zijazobaadae katika uwanja wa nyimbo za Siti binti Saad katika vipengele vyengine vya fani na maudhui kama vile matumizi ya lugha kwa upana zaidi, muundo, falsafa, ujumbe na maadili, mtazamo na msimamo.

Item Type: Thesis (Masters)
Subjects: 400 Language > 490 Other languages
Divisions: Faculty of Arts and Social Sciences > Department of Linguistics and Literary Studies
Depositing User: Mr Habibu Kazimzuri
Date Deposited: 24 May 2017 08:26
Last Modified: 24 May 2017 08:26
URI: http://repository.out.ac.tz/id/eprint/1853

Actions (login required)

View Item View Item