Viambishi njeo katika vitenzi vya lahaja ya Kipemba : Uchanganuzi wa kimofofonolojia kuonesha muundo ndani na muundo nje

Abdulla, Halima Salim (2016) Viambishi njeo katika vitenzi vya lahaja ya Kipemba : Uchanganuzi wa kimofofonolojia kuonesha muundo ndani na muundo nje. Masters thesis, The Open University of Tanzania.

[thumbnail of HALIMA_SALIM_ABDULLA.pdf]
Preview
PDF - Submitted Version
Download (414kB) | Preview

Abstract

Kazi hii inachambua mofofonolojia ya vitenzi vya lahaja ya Kipemba kuonesha muundo ndani na muundo nje . Utafiti ulilenga ubainisha mambo matatu; kwanza kuchunguza viambishi njeo katika vitenzi vya lahaja ya Kipemba; pili kueleza michakato ya kimofofonolojia inayojitokeza katika kubadilisha miundo ndani na miundo nje; na tatu kudhihirisha kanuni zinazotawala mabadiliko ya muundo ndani na muundo nje katika vitenzi vya lahaja ya Kipemba. Utafiti huu ulifanyika katika Shehia ya Mtambwe Kaskazini katika jimbo la Mtambwe ambalo lilihusisha kijiji cha Kele, Uondwe, Mpakanjia, Jambaji, Kiapaka na Chanjaani. Watoa taarifa za utafiti walikuwa wakaazi asilia wa Mtambwe Kaskazini wenye umri kati ya miaka sitini nakuendelea ambao waliteuliwa kumi kutoka kila kijiji kwa njia ya usampulishaji bahati nasibu. Mbinu mbalimbali za utafiti zilitumika katika utafiti huu zikiwemo mbinu ya dodoso, usaili na uchunguzi makini. Matokeo ya utafiti yameonyesha michakato ya kimofofonolojia inavyojitokeza kwenye mabadiliko kutoka muundo ndani kwenda muundo nje katika vitenzi vya lahaja ya Kipemba na kubainisha kanuni zinazotawala mabadiliko yanayotokea kutoka muundo ndani kwenda muundo nje katika vitenzi vya lahaja za Kipemba.

Item Type: Thesis (Masters)
Subjects: 400 Language > 490 Other languages
Divisions: Faculty of Arts and Social Sciences > Department of Linguistics and Literary Studies
Depositing User: Mr Habibu Kazimzuri
Date Deposited: 01 Mar 2017 08:09
Last Modified: 23 May 2017 09:19
URI: http://repository.out.ac.tz/id/eprint/1712

Actions (login required)

View Item View Item