Kuchunguza sababu za upungufu wa istilahi za Kiswahili za kufundishia sayansi na teknolojia katika shule za msingi: Mfano wa kisiwani cha Pemba

Nassor, Fakih Mkubwa (2017) Kuchunguza sababu za upungufu wa istilahi za Kiswahili za kufundishia sayansi na teknolojia katika shule za msingi: Mfano wa kisiwani cha Pemba. Masters thesis, The Open University of Tanzania.

[thumbnail of FAKIH_MKUBWA_NASSOR.pdf]
Preview
PDF - Submitted Version
Download (432kB) | Preview

Abstract

Lengo kuu la utafiti huu lilikuwa ni kuchunguza sababu zinazopelekea upungufu wa istilahi za Kiswahili za kufundishia sayansi na teknolojia. Lengo hili limeweza kufanikiwa kwa kukamilika kwa malengo mahususi matatu ya utafiti, ambayo ni; kubainisha sababu zinazopelekea upungufu wa istilahi za Kiswahili za kufundishia sayansi na teknologia katika shule za msingi Pemba; kueleza matatizo yanayowakabili walimu na wanafunzi wa shule za msingi kutokana na uwepo wa upungufu wa istilahi za Kiswahili za kufundishia sayansi na teknolojia na; kuelezea jinsi walimu na wanafunzi wanavyokabiliana na upungufu wa istilahi hizo. Maandiko na mapito mbalimbali yahusianayo na mada yamepitwa. Utafiti huu uliongozwa na nadharia mbili ambazo ni Nadharia za jumla ya Istilahi na Nadharia za kisayansi ya Istilahi. Mbinu za dodoso na usaili zilitumika katika ukusanyaji wa data. Utafiti ulifuata muundo mseto ambao ulihusisha muundo wa kitakwimu na muundo wa kiidadi katika uchanganuzi wa data. Matokeo ya utafiti yameonyesha kwamba kuna sababu mbalimbali zinazopelekea upungufu wa istilahi za Kiswahili za kufundishia sayansi na teknolojia, vilevile matokeo yameonesha matatizo mbalimbali yanayowakabili walimu na wanafunzi kutokana na uwepo wa upungufu wa istilahi za Kiswahili za kufundishia sayansi na teknolojia. Pia matokeo ya utafti yameonesha njia mbalimbali ambazo walimu na wanafunzi wanatumia katika kukabiliana na tatizo hili la upungufu wa istilahi za kufundishia sayansi na teknolojia katika lugha ya Kiswahili. Kwa mujibu wa data zilizopatikana, utafiti umetoa mapendekezo kuhusu baadhi ya maeneo ambayo yanahitaji kufanyiwa utafiti na baadhi ya maeneo ambayo yanahitaji kuchukuliwa hatua za kiutendaji.

Item Type: Thesis (Masters)
Subjects: 400 Language > 490 Other languages
Divisions: Faculty of Arts and Social Sciences > Department of Linguistics and Literary Studies
Depositing User: Mr Habibu Kazimzuri
Date Deposited: 01 Mar 2017 08:10
Last Modified: 23 May 2017 09:14
URI: http://repository.out.ac.tz/id/eprint/1699

Actions (login required)

View Item View Item