Ulinganishi Changanuzi wa Mofu Njeo za Kikara na Kiswahili

Magesa, January Peter Nyawema , (2017) Ulinganishi Changanuzi wa Mofu Njeo za Kikara na Kiswahili. Masters thesis, The Open University of Tanzania.

[thumbnail of TASINIFU_YA_Magessa-21-01-2017.pdf]
Preview
PDF - Submitted Version
Download (1MB) | Preview

Abstract

Lengo la utafiti huu lilikuwa kuchunguza, kubaini na kulinganisha mofu njeo za kitenzi cha Kikara na za Kiswahili ili kujua idadi yake, mazingira zinapotokea na athari ya maumbo yake inayotokana na mazingira zilimo. Utafiti huu ulifanywa katika kata za Bukiko na Nyamanga wilaya ya Ukerewe kwa kuwatumia watoa habari 45 waliosailiwa na kujibu maswali. Utafiti huu umetumia nadharia ya Ulalo ya Reichenbach ambayo huchunguza, hubainisha na kulinganisha mofu njeo katika lugha ya Kikara na Kiswahili. Aidha nadharia hii inahusisha maumbo ya mofu njeo kwa kuonyesha wakati uliopita, wakati uliopo na wakati ujao. Mbinu ya utafiti iliyotumika katika kukusanya data ilikuwa ni usaili na dodoso. Katika utafiti huu watoa taarifa waliteuliwa kwa kuzigatia kigezo cha usampulishaji lengwa na nasibu. Uchambuzi wa data ulibainisha kuwa lugha zilizochunguzwa zilikuwa na idadi tofauti ya mofu njeo. Kikara kina jumla ya mofu njeo saba ilihali Kiswahili kina mofu njeo tano. Utafiti huu uligundua mazingira ya kutokea kwa mofu njeo hizi katika vitenzi yalikuwa tofauti kwa baadhi ya mofu njeo na kufanana kwa mofu nyingine. Aidha maumbo ya mofu katika vitenzi yaliathiriwa na mazingira yalimokuwa, ambazo husababishwa na muungano wa irabu zinazokabiliana katika kingo zake.

Item Type: Thesis (Masters)
Subjects: 400 Language > 490 Other languages
Divisions: Faculty of Arts and Social Sciences > Department of Linguistics and Literary Studies
Depositing User: Mr Habibu Kazimzuri
Date Deposited: 14 Feb 2017 12:34
Last Modified: 17 Oct 2018 14:52
URI: http://repository.out.ac.tz/id/eprint/1611

Actions (login required)

View Item View Item