Kuchunguza Kiwango cha Mabadiliko ya Matumizi ya Msamiati wa Kipemba

Suleiman, Kauthar Abdalla (2015) Kuchunguza Kiwango cha Mabadiliko ya Matumizi ya Msamiati wa Kipemba. Masters thesis, The Open University Of Tanzania.

[thumbnail of KAUTHAR_ABDALLA_SULEIMAN_.pdf]
Preview
PDF
Download (937kB) | Preview

Abstract

Utafiti huu ulikuwa na lengo la “Kuchunguza Kiwango cha Mabadiliko ya Matumizi ya Msamiati wa Kipemba katika Muktadha wa Harusini, Msibani, Uvuvini na Kilimoni”. Malengo ya utafiti yalikuwa; (i) Kuainisha msamiati wa harusini, msibani, uvuvini na kilimoni unaotumika katika lahaja ya Kipemba. (ii) Kutathmini tofauti ya kiasi cha mabadiliko ya matumizi ya msamiati huo. na (iii) kuchunguza sababu zilizosababisha mabadiliko ya matumizi ya msamiati wa Kipemba. Utafiti huu umeongozwa na nadharia ya Foucault (1981) ya Mwenendo na Mabadiliko. Nadharia ya Darwin (1838) ya Ubadilikaji na Nadharia Kidhi ya Mawasiliano (NKM) ya Giles ya mwaka (1991). Jumla ya watafitiwa 87 walishiriki katika utafiti huu. Data zilikusanywa kwa kutumia mbinu ya hojaji, usaili na maelezo. Pia data ziliainishwa kwa njia ya kiidadi (kitakwimu) na isiyo ya kiidadi (maelezo). Utafiti umeonesha kuwa; (i) Msamiati wa muktadha wa harusini umebadilika zaidi kuliko miktadha mingine mitatu sawa na 33.33%. (ii) Msamiati wa kilimoni na uvuvini ukifuatia sawa na 22.81% kwa kila muktadha. (iii) Utafiti umegundua kuwa msamiati wa msibani umebadilika kwa kiwango kidogo wastani wa 21.05%. Sababu za mabadiliko hayo tafiti imeonesha ni kukua kwa sayansi na teknolojia, matumizi ya utandawazi pamoja na vyombo vya mawasiliano, kuwepo kwa lahaja iliyorasmi, athari ya maendeleo ya watu kuhamahama, mabadiliko ya kiutamaduni, maingiliano ya kindoa na misimamo ya kidini. Utafiti huu unapendekeza, msamiati wa Kipemba uendelee kutumika kwani unasaidia kuwatambua watu wenye asili hiyo na kujaza pengo la istilahi za Kiswahili na msamiati wa Kipemba ni amana na hazina ya lugha yetu uhifadhiwe vizuri ili amana hii ya lugha isipotee.

Item Type: Thesis (Masters)
Subjects: 400 Language > 490 Other languages
Divisions: Faculty of Arts and Social Sciences > Department of Linguistics and Literary Studies
Depositing User: Mr Habibu Kazimzuri
Date Deposited: 13 Jul 2016 10:15
Last Modified: 13 Jul 2016 10:15
URI: http://repository.out.ac.tz/id/eprint/1400

Actions (login required)

View Item View Item