Athari za Lugha ya Kinyamwezi Katika Kujifunza Lugha ya Kiswahili

Nyanda, Josephine (2015) Athari za Lugha ya Kinyamwezi Katika Kujifunza Lugha ya Kiswahili. Masters thesis, The Open University Of Tanzania.

[thumbnail of Dissertation_-_NYANDA_JOSEPHINE_-_Final-1.pdf]
Preview
PDF
Download (365kB) | Preview

Abstract

Utafiti huu ulikuwa na lengo la kuchunguza Athari za Kinyamwezi Katika Kujifunza Lugha ya Kiswahili.Umetumia nadharia ya Fonolojia Zalishi Asilia ili kuweka bayana athari hizo. Sura ya Kwanza imeshughulikia Utangulizi, Tatizo la Utafiti, Malengo ya Utafiti, Umuhimu wa Utafiti, Mawanda na Mipaka ya Utafiti na Mpango wa Utafiti.Sura ya Pili imeshughulikia Mapitio ya Kitaaluma na ya Kazi Tangulizi ambapo imeelezea yaliyoandikwa kuhusu lugha na athari za lugha za kibantu katika Ujifunzaji wa Lugha ya Kiswahili.Aidha, imeelezea yaliyoandikwa kuhusu Ala za Sauti, Sauti za Lugha, Namna ya Utamkaji na Mahali pa Kutamkia Sauti za Kiswahili. Imeelezea Pengo la Maarifa na Kiunzi cha Nadharia. Sura ya Tatu imezungumzia Njia na Mbinu za Utafiti.Imezungumzia Utangulizi, Eneo la Utafiti, Sampuli ya Utafiti na Usampulishaji,Vyanzo vya Data,Ukusanyaji wa Data, Mkabala wa Uchambuzi wa Data,Uchambuzi wa Data na Vikwazo vya Utafiti.Sura ya Nne imeeleza juu ya Uwasilishaji na Uchambuzi wa data,ambapo imeelezea aina za fonimu za Kinyamwezi na Athari ya Lugha ya Kinyamwezi katika Kujifunza Lugha ya Kiswahili. Sura ya tano imeeleza juu ya Muhtasari wa Utafiti na Mapendekezo.

Item Type: Thesis (Masters)
Subjects: 400 Language > 490 Other languages
Divisions: Faculty of Arts and Social Sciences > Department of Linguistics and Literary Studies
Depositing User: Mr Habibu Kazimzuri
Date Deposited: 13 Jul 2016 10:25
Last Modified: 13 Jul 2016 10:25
URI: http://repository.out.ac.tz/id/eprint/1352

Actions (login required)

View Item View Item