Kuchunguza Mtindo katika Nyimbo za Tiba Asili: Mifano Kutoka Nyimbo za Waganga wa Mkoa wa Ruvuma

Migodela, Willy (2020) Kuchunguza Mtindo katika Nyimbo za Tiba Asili: Mifano Kutoka Nyimbo za Waganga wa Mkoa wa Ruvuma. ["eprint_fieldopt_thesis_type_phd" not defined] thesis, The Open University of Tanzania.

[thumbnail of WILLY MIGODELA TASNIFU.pdf] PDF
Download (9MB)

Abstract

Utafiti huu ulihusu ‘Kuchunguza Mtindo katika Nyimbo za Tiba Asili: Mifano Kutoka Nyimbo za Waganga wa Mkoa wa Ruvuma’. Utafiti ulikuwa na malengo mahsusi matatu. Lengo mahsusi la kwanza lilihusu kuainisha nyimbo za tiba asili za waganga wa mkoa wa Ruvuma. Lengo mahsusi la pili lilihusu kubainisha mtindo wa nyimbo za tiba asili za waganga wa mkoa wa Ruvuma. Lengo la tatu lilikuwa ni kutathmini matokeo ya mtindo wa nyimbo za tiba asili kwa wagonjwa. Utafiti huu uliongozwa na nadharia mbili za Mitindo na Simiotiki, pamoja na mbinu ya maelezo ya kinathari. Matokeo yanaonesha kwamba, kuna aina saba za nyimbo za tiba asili zinazotokana na dhima ya nyimbo hizo. Aina hizo ni nyimbo za maombi, kuomboleza, kufurahisha mizimu, kueleza historia, shkurani, kutolea tiba na nyimbo za kuaga. Vilevile, kuna mitindo mbalimbali inayotokana na matumizi na viziaadalugha. Mitindo hiyo, inahusiana na matumizi ya lugha ya kawaida na lugha ya kisanaa namatumizi ya nyimbo ndefu na fupi. Pia, kuna mishororo, fomula, dailojia, vina na mizani, uchezaji, utendaji wa kimuziki na matumizi ya maleba na vifaa. aidha, upo uhusiano wa moja kwa moja baina ya nyimbo na matibabu katika tiba asili. Matokeo ya nyimbo hizo kwa wagonjwa yamebainika kuwa ni pamoja na kuwatia moyo wagonjwa, kuwashirikisha katika mchakato wa tiba, kuburudika, kuwaongezea imani ya tiba na kufukuza majini wabaya. Utafiti huu ni kwamba, serikali ibuni sera za kuwaendeleza waganga wa tiba asili na kutoa kipaumbele kwenye tafiti za kitamaduni ili kulinda amali za taifa. Watafiti wengine wanaweza kufanya tafiti zaidi kuhusu maudhui ya nyimbo za

Item Type: Thesis (["eprint_fieldopt_thesis_type_phd" not defined])
Subjects: 800 Literature > 800 Literature, rhetoric & criticism
Divisions: Faculty of Arts and Social Sciences > Department of Linguistics and Literary Studies
Depositing User: Mr. Administrator OUT
Date Deposited: 22 Sep 2021 10:09
Last Modified: 22 Sep 2021 10:09
URI: http://repository.out.ac.tz/id/eprint/2949

Actions (login required)

View Item View Item