Kuchunguza Dhima za Methali Zinavyoendeleza Elimu ya Jadi. Mfano Kutoka Jamii ya Wapare wa Shighatini Mwanga

Hatibu, Sadi (2017) Kuchunguza Dhima za Methali Zinavyoendeleza Elimu ya Jadi. Mfano Kutoka Jamii ya Wapare wa Shighatini Mwanga. Masters thesis, The Open University of Tanzania.

[thumbnail of TASNIFU - SADI HATIBU.pdf]
Preview
PDF - Submitted Version
Download (4MB) | Preview

Abstract

Utafiti huu unahusu Kuchunguza Dhima za Methali zinavyoendeleza Elimu ya jadi. Mfano Kutoka Jamii ya Wapare wa Shighatini Mwanga. Utafiti huu umeongozwa na nadharia ya Fasihi Ina Kwao. Kwa upande wa mbinu za kukusanyia data, mtafiti ametumia mbinu ya umakinifu, usaili, hojaji, kusoma machapishi na wasaidizi katika kukusanya data. Matokeo ya utafiti huu yanaonesha kuwa, kundi la watu, wanaozingatia mila na dasturi za Kipare, ikiwa ni pamoja na matumizi ya methali za Kipare wanakuwa na maadili mazuri. Imebainika kuwa, kumekuwa na kushuka kwa maadili katika jamii ya Wapare kwa kadiri siku zinavyosonga mbele. Hali hiyo imesababishwa na hali ya vijana wengi kupuuza mila za Kipare na wazee kutotia juhudi kubwa katika kuzirithisha mila zao kwa vijana wao. Pamoja na kuwapo kwa matumizi ya methali katika baadhi ya shughuli za kimila, matumizi hayo hayatoshelezi mahitaji ya jamii na hivyo, kuchangia kushuka kwa maadili mema. Kazi hii ya utafiti imeziainisha methali katika makundi kulingana na uelekeo wa dhima zake, kama ilivyofafanuliwa, katika sura ya nne ya utafiti huu. Dhima kuu ya methali hizo imeonekana kuwa, ni kuielimisha jamii. Makundi mengine yaliyoainishwa ni methali zinazohimiza uwajibikaji na kuepuka uvivu, methali za kuwatakia watu kheri na baraka, methali za kuwalaani watendao maovu, methali za kuhadharisha na kuelekeza, methali zinazotaja utu wema na uhusiano mzuri, na kundi jingine ni la methali, zinazozungumzia uhusiano na ushirikiano. Kila taifa linahakikisha, jamii ya watu wake, inakuwa katika hali ya amani, utulivu na maadili mema. Kulingana na methali zilizochambuliwa, nyingi zimegusa masuala hayo ya maadili mema kwa jamii. Hivyo, methali zinaonekana kuwa nguzo muhimu, kwenye ustawi wa maisha ya kila siku ya jamii.

Item Type: Thesis (Masters)
Subjects: 400 Language > 490 Other languages
Divisions: UNSPECIFIED
Depositing User: Mr Habibu Kazimzuri
Date Deposited: 05 Oct 2018 17:30
Last Modified: 05 Oct 2018 17:30
URI: http://repository.out.ac.tz/id/eprint/2124

Actions (login required)

View Item View Item